Tuesday, May 23, 2017

Published 5/23/2017 01:54:00 PM by

BASATA WAUTA BEN POLMTAF

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania, BASATA, Godfrey Mngereza amelaani picha za nusu za utupu za msanii wa muziki, Ben Pol ambazo imezua tafrani kubwa kwenye mitandao ya kijamii.
Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Mngereza amewataka wasanii kufanya kazi nzuri ambazo zinaweza kuwaweka sehemu nzuri na siyo kutengeneza mazingira ambayo yanautia dosari muziki wao.


“Sisi kama BASATA tumeona hizo picha mtandaoni, siyo kitu kizuri, kwanza hakiendani na tamaduni zetu. Kwahiyo sisi tunamtafuta Ben Pol halafu tumsikilize, atueleze zile picha ilikuwaje mpaka zikasambaa mitandaoni. Tukiongea naye tunaweza kutoa kauli yoyote na kulaani matukio ya namna hiyo,”
Aliongeza,” Pia naungana na wasanii waliolaani kitendo hiko ambacho ni cha ajabu sana na baraza kwa mamlaka yake kama mzazi haiwezi kukaa kimya lazima tujue kama ana tatizo la akili au maadili limemkumba Ben Pol.”
Pia Mngereza amewaomba wasanii wa Tanzania kwa upande wa muziki wafanye muziki mzuri wasitegemee kiki.


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Read More
      edit
Published 5/23/2017 01:39:00 PM by

RUGE AJIBU KEJERI ZA MKUU WA MKOA



Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, (pichani) amejibu kauli za kejeli zilizotolewa na Mkuu wa Mkoa (RC) wa Dar Dar es Salaam ya kuwa yeye ni muongo na anafaa tu kuwa mwandishi wa mashairi na nyimbo za mapenzi na ngonjera.
Ruge ametoa kauli hiyo jana katika Kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na kituo hicho, ambapo walikuwa na kipindi cha ‘Shukrani’ kwa wasikilizaji wao na watu waliowahi kuwasaidia kupata misaada. “Kila mtu ana mtazamo wake, na huwezi kulazimisha mtazamo wa mtu ubadilike. Inasikitisha sana kuona mtu anayesambaza haya mambo ni bosi wangu, bosi wa mkoa wetu. Yeye akipiga muhuri kitu ndiyo imekaa hiyo, yeye ana nguvu zote,” alisema Ruge.
“Sasa akisema hivyo mimi ni tapeli anataka kila mtu Dar es Salaam anione hivyo. Mimi sina nguvu kwa hiyo nachagua kubaki kwenye ninachokiamini. Tangu mwanzo nilisema mimi nataka haya mambo yaishe, cha kusikitisha huyu mtu ni kiongozi lakini anashindwa kumaliza jambo hili kwa busara na anataka kuliendeleza.

“Kuna mambo hapa najaribu kutengenezwa. Watu wanajaribu kutusukuma turudi kwenye mjadala ambao tulishaumaliza. Mimi ni mtu mzima na busara inaniambia watu wazima hatuna haja ya kurudi kwenye majibizano ambayo kwangu yaliisha siku nyingi,” alisema Ruge.
Hata hivyo, kipindi hicho kilikatizwa ghafla kwa sababu ambazo hazijajulikana. Mkuu wa Mkoa wa Dar jana alihojiwa ‘laivu’ na kituo kimoja cha televisheni ambapo baadhi ya maswali aliyoulizwa likiwemo la jina, hakujibu

Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa



 CHANZO:GPL
Read More
      edit

Friday, May 19, 2017

Published 5/19/2017 07:19:00 PM by

NDUGU WA HARMORAPA HUYU HAPA



Kijana mmoja aliyesema anaitwa Frank Omary amesafiri kutoka Iringa kuja Dar kumtafuta Harmorappa mna kudai yeye ni ndugu yake mama yake amemwambi ni wa baba mmoja, ameacha na namba zake akitaka Harmorapa amtafute akiona ujumbe wake mtandaoni.


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Read More
      edit
Published 5/19/2017 05:08:00 PM by

WEMA KWA HILI HAKUNA WA KUKUOA

Hii siyo mara yangu ya kwanza kumzungumzia Wema katika safu hii na kwa maana hiyo, sitarudia kuzitaja sifa zake nyingi katika uigizaji wa fi lamu. Na siyo kwamba ninakutana naye hapa mara nyingi kwa sababu nina chuki naye, hapana, huwezi kuwa na chuki na mtu kama Wema, ambaye ni mkarimu kwa kila mtu, uongo?
Huyu binti ni role model wa watu wengi sana, wake kwa waume na katika akaunti yake ya Instagram, ana wafuasi zaidi ya milioni moja. Hao ni watu wengi mno, ina maana akitaka kuhamasisha kitu, wanaweza kutoa ushawishi kwa idadi nyingine kama hiyo na kitu kikasimama.



Kwa maana hiyo, mtu kama huyu ni rahisi kuweka mwelekeo anaoutaka, ndiyo maana akapata hata jeuri ya kuanzisha App yake na watu kibao wanaifuatilia. Juzi hapa nimeona kitu Wema ameandika katika akaunti yake ya Instagram, anawataka mashabikiwake wakubali ukweli kuwa yeye hivi sasa hana mpenzi, kwani uhusiano wa kimapenzi aliokuwa nao zamani, hivi sasa umeisha kwani kila mmoja ana maisha yake.
Lakini aliponikosha ni pale aliposema anawaomba wamuombee kwa Mungu apate mwanaume mzuri wa kuweza kumuoa, tena mwanaume huyo awe na mihela miiiingi!
Hapo kwenye mihela mingi ndipo paliponitatiza. Nimewahi kusema huko nyuma, kuwa Wema kwa kule majuu, unaweza kumfananisha na binti mmoja anaitwa Kim Kardashian, mtangazaji wa televisheni ambaye pia ni mke wa rapa mashuhuri duniani, Kanye West. Kuna watu wanamsema binti huyu wa Kinyaturu kuwa eti ‘ametoka’ na wanaume wengi.
Kwa taarifa yao ni kuwa Kim, kabla ya kuangukia mikononi mwa West, alishatoka na mastaa zaidi ya 25, achilia mbali wale ambao hawaeleweki. Huu ni umri wa Wema kutafuta mume mwenye busara wa kumuoa na siyo mwenye fedha kwa sababu hawa wenye mkwanja mbona amesha-hag nao sana tu? Kila mmoja anajua kuwa ili kutoka na supastaa Wema ni lazima uwe na waleti iliyonona, siyo kwa ajili ya kumpa, bali kwa sababu ya gharama za kum-handle


Nilidhani angetumia nafasi ile kuwaomba mashabiki wake, wamuombee kwa Bwana Mungu wake, ampate mume bora wa kumuoa ambaye ni mwenye hofu ya Mungu, busara, hekima na upendo, maana ndicho kitu cha msingi zaidi mwanamke anakihitaji kutoka kwa mwanaume anayempenda.
Mwanamke anayetafuta mwanaume mwenye hela, hawezi kumpata wa kumuoa, bali wa kumchezea tu kwa sababu wenye hela hawajui kupenda, atapenda wangapi wakati kila mrembo anamhitaji? Wanaume wengi wenye hela huoana na wapenzi wao walioanza nao kuhangaika pamoja, hawa wengine wanaojitokeza huku juu, huwa ni wa kupotezea tu wakati.

Hivyo nikupe ushauri mdogo wangu, kwanza umri wako wa kuolewa umeshafi ka, ni vyema na haki sasa ukatafuta mtu wa kutuliza naye mpira. Pili, usiwaze sana kuhusu hela, zinatafutwa na wewe unao uwezo wa kuzipata, ukazitumia na mumeo. Umekutana na wanaume wengi wenye nazo na wewe ukazitumia sana, hukuwekeza ili zikufae ndiyo  utampa wakati huu?


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

CHANZO: GPL
Read More
      edit
Published 5/19/2017 04:55:00 PM by

KUTOKA MSIBANI WA DOGO MFAUME

KUFUATIA kifo cha aliyekuwa Msanii wa Bongo Fleva, Mfaume Selemani ‘Dogo Mfaume’, aliyetamba zaidi na wimbo wake wa Kazi ya Dukani kufariki dunia juzi Mei 17, 2017, mwili wa marehemu unatarajiwa kuzikwa leo .














Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

CHANZO: GPL
Read More
      edit

Thursday, May 18, 2017

Published 5/18/2017 10:02:00 PM by

INAWEZEKANA KUITIBUA NDOA YAKO KWA MAVAZI YA KISASA?

Ni wiki nyingine tena tunakutana kupitia safu hii nikiamini kwamba umzima na unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku kama kawaida. Kwa upande wangu namshukuru Mungu kwa kunijaalia siha njema kiasi cha kuniwezesha kuwa nanyi tena kupitia safu hii ambapo tunaelimishana na kukumbushana juu ya mambo mbalimbali yanayogusa maisha yetu.
Wiki hii nataka kuzungumzia suala la mavazi hasa kwa watu walio kwenye ndoa. Bila shaka ilishawahi kutokea siku moja mwenza wako akavaa mavazi ambayo hayakukufurahisha, aidha kutokana na ‘urafu’ wake kiasi cha kuweza kuonekana kituko mbele za watu ama alivaa nguo zisizo za heshima zinazoweza kuwafanya watu wakamtafsiri tofauti.
Kama haijawahi kukutokea, binafsi nimeshuhudia wanandoa wakitibuana kwa sababu tu mwanaume amekuwa akimtaka mkewe kubadili staili ya uvaaji wake lakini mke amekuwa aking’ang’ana na mavazi yaleyale ambayo mumewe hayapendi kwa maelezo kuwa, ndiyo aliyozoea kuyavaa.
Kwa wanawake kuna hili suala la kwenda na wakati, kuna mitindo mingi ya nguo imeingia baadhi ikiwa haina matatizo lakini kiukweli kuna mavazi ambayo yamekuwa yakileta mtafaruku mkubwa kwa wanandoa wenye msimamo.
Sikatai kuna uhuru wa mtu kuchagua avae nini akienda wapi lakini kuna mavazi mengine inatakiwa kutumia busara kabla ya kuyaweka mwilini.
Katika hili kabla sijaitumia siku nyingine kuwazungumzia wanaume, nianze na wanawake ambao ndiyo wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutoithamini miili yao na kujikuta wakivaa mavazi yanayoacha wazi sehemu ambazo katika hali ya kawaida zilistahili kuonwa na wapenzi wao tu.



Kuna wanaume wasiopenda kuwaona wake zao wakiwa wamevaa suruali zinazobana na vitopu, vimini na nguo nyingine za kihasara lakini wakati huohuo unakuta mwanamke amezoea kuvaa mavazi hayo tangu alipokuwa mdogo na hakuona tatizo lolote, leo hii ukimwambia asivae mavazi hayo nini kinaweza kutokea?
Naamini mwanamke ataona ananyimwa uhuru wake wa kuchangua na kuhisi ameingia kwenye ndoa na mwanaume ‘anayemaindi vitu vidogo’ lakini je, mke anaweza kuikimbia ndoa eti kwa sababu tu amekatazwa kuvaa suruali wakati yeye amezoea? Ni vigumu na kama atafanya hivyo, huyo atakuwa na matatizo.
Ninachotaka kusema ni kwamba, ndoa inanoga pale ambapo kuna maelewano kati ya wawili waliotokea kupendana. Hivi inapotokea mwenza wako akakueleza kwamba hapendi kukuona umevaa mavazi f’lani kuna ugumu gani kubadilika?
Huoni kwamba kwa kufanya hivyo licha ya kumfurahisha pia ataona unamheshimu na kumsikiliza?
Wanawake wakae wakijua kwamba kinachowafanya wanaume kufi kia hatua ya kuwakataza wao kuvaa aina f’lani ya mavazi katika maeneo f’lani ni wivu na kulinda heshima ndiyo maana naweza kusema kwamba, ukiwa na mtu ambaye hata ukivaa nguo inayoacha wazi matiti na mapaja anachukulia poa tu, huyo hana wivu na wala hakujali.
Achana na ulimbukeni wa kusema eti unakwenda na wakati, waache wale walio nje ya ndoa, wanaojiuza, walioingia katika uhusiano na wanaume wasiojali waendelee kwenda na wakati kwa kuvaa mavazi ambayo hayawezi kuwafanya waheshimike.
Wewe msome mwenza wako na kubaini aina ya mavazi anayopenda kukuona ukiwa umeyavaa. Kuna wanawake wengine hasa wale walio ndani ya ndoa wana tabia ya kuvaa kanga moja tu kisha kukatiza mtaani huku wakitingisha makalio yao tena mbele za wanaume, ili iweje sasa?
Wakutongoze au? Mbona mambo mengine ni kutumia akili tu jamani?
Nihitimishe kwa kusema kwamba, ukiwa chumbani na mumeo vaa upendavyo. Lakini pale unapotoka akikisha unavaa mavazi ambayo hayatamkera.
Ukifanya hivyo kwanza utajijengea heshima lakini pia utamtunzia heshima mumeo na hakika kwa kufanya hivyo utaijengea ndoa yako mazingira ya kudumu. Ushauri wangu ni kwamba, epuka kujifanya unakwenda na wakati katika suala la uvaaji wakati unaiweka rehani ndoa yako.



 Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

CHANZO: GPL
Read More
      edit
Published 5/18/2017 04:20:00 PM by

SIRI YA UTAJIRI

Siri kubwa ya utajiri ni kujifunza elimu ya namna ya kutafuta mtaji. Kuwekeza kwa busara kwa namna ambayo daima panakuwa na ziada na faida.Hivyo kuelekea ukwasi ni kubuni maradi endelevu, yaani unaweza kuitoa ziada na faida.


 Pia mkujifunza na kuweza tabia ya kuweka akiba na kuwekeza fedha hizo za akiba katika vitega uchumi ambavyo vinazalisha faida endelevu.Pamoja na kujifunza namna ya kufanya biashara na kuanzisha biashara yako ili iwe endelevu.


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Na.M&U

Read More
      edit
Published 5/18/2017 01:17:00 PM by

AMBER LULU ACHA UCHAFU WA MAPICHA, FANYA MUZIKI


NIANZE kumsh-ukuru Mungu kwa kila jambo katika maisha yangu na yako msomaji wa Barua Nzito, hasa baada ya kumaliza wiki ngumu na ya majonzi kwa Watanzania wote kupatwa na msiba mkubwa wa kufiwa na wanafunzi 32 kwa wakati mmoja.
Kama mwanajamii, nina kila sababu ya kutoa maoni yangu kwa jamii na wanajamii wenyewe katika kushauri juu ya mazuri au mabaya wanayofanya. Leo hii nimeandika waraka maalumu kwa rafiki na dada yangu mpendwa, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’ aliyeanza kutambulika kwenye baadhi ya video za wasanii wa Bongo Fleva kama ‘video queen’ ikiwemo Usimsahau Mchizi ya R.O.M.A, Inde ya Dully Sykes na nyingine kibao.




Kama ilivyo kawaida maisha ni kupanda na kuongeza kitu kila kukicha, nashukuru rafiki yangu, Amber Lulu ameongeza wasifu mwingine wa kuwa msanii wa Bongo Fleva, tayari ameachia ngoma ya Watakoma aliyomshirikisha mkali wa kurap, Country Boy. Inafanya vizuri, imepenya, ni ngoma ambayo inachezeka na kama unapenda kuicheza na hata ukitembelea baadhi ya kumbi za starehe utasikia inachezwa.





Simzungumzii Amber Lulu kwa kujifananisha na Amber Rose wa Marekani, simzungumzii kwa kufanana kiana na kuiga mtindo wake wa nywele, ‘kujibinua’ kama wanavyofanya watoto wa mjini kwa sasa, kwa sababu kuiga mtu si vibaya kama utaiga mazuri yake, ila ukiiga mabaya basi utaonekana wa ajabu sana.
Kiukweli Amber unakera dada yangu kwa tabia yako ya kupiga picha za ajabu, juzikati nimeona picha ambayo umechuchumaa mbele ya mwanaume kama unafungua sehemu ya zipu yake vile. Nikiwa bado natafakari kuhusu picha hiyo, ghafla naona picha nyingine ukiwa umemshika sehemu nyeti mwanamke mwenzako.
Nini tafsiri ya picha hizi mbili? Umelenga kufikisha ujumbe gani kwa jamii? Kwamba unashiriki mapenzi ya jinsia moja au umepinda kupindukia, au ndiyo ‘kitu cha Arusha’ kinafanya kazi yake.







Najaribu kuvaa uhusika wa mimi kama baba, kaka au ndugu yako wa kiume halafu naona picha zako za utupu mitandaoni unadhani nitajisikiaje, nitawaza nini juu yako?
Hivi Amber kama una wazazi wako unahisi unawaweka kwenye wakati gani huko wanakoishi, mbaya zaidi picha zilizoko mitandaoni si kwamba zimepigwa kwa kuibia au bahati mbaya la hasha, si kweli kwamba zimepostiwa na wabaya wako kwa kusudi la kukuchafua ni picha ulizojiandaa kwa pozi za uchafu huo kisha ukaziposti mitandaoni.
Waswahili wanasema akili za kuambiwa changanya na za kujiongeza, Amber umekuwa ukifanya mambo ya ajabu kwa sababu ya kumuiga ‘role model’ wako, Amber Rose wa Marekani, lakini unasahau kuwa Afrika na Marekani ni vitu viwili tofauti, kuna mambo yakifanyika kule au kwingineko huonekani wa ajabu lakini mambo hayohayo ukiyafanya kwetu unaonekana ni mwendawazimu.





Rafiki yangu mbona unajiabisha hivyo, kwa nini usijikite zaidi kwenye kufanya muziki kuliko kupiga picha za uchafu na kutupia mitandaoni.
Nakukubali sana kwenye muziki lakini kwenye mapicha ya uchafu siko nawe, nikisema nakukubali namaanisha na hata siku za nyuma niliandika makala inayosema
VITA YA WAUZA SURA WA KIBONGO, ndani ya makala hayo nilizungumzia vita yako na Gigy Money na Lulu Diva kuanzia kwenye video queen hadi kuwa wanamuziki na nikachambua kuwa mtu ambaye nyota yake inaonekana kung’ara kwenye muziki ni wewe, sina nia mbaya ya kukupaka matope lakini kwa hili la mapicha ya ajabu acha tu nikupake.




Mapicha picha hayo si tu nimeyaona mtandaoni lakini hata maisha yako ya kawaida yamejaa ulimbukeni fulani hivi. Nakumbuka hata kwenye bethidei yako iliyofanyika Bunju nje kidogo ya Jiji la Dar ulikata mauno ya ajabu kwa kushika meza na kufanya kila aina ya mbwembwe.
Sikatazi usicheze ila cheza kwa staha, unachokifanya ni ushamba, ulimbukeni, ni kushindwa kufikiria nje ya boksi kuwa kuna maisha nje ya sanaa ya mapichapicha machafu.


Nilibahatika pia kusikilia mahojiano yako na kituo kimoja cha redio, Amber hata watangazaji waliokuhoji walikuambia kuwa kati ya video queen walioachia ngoma zao ni wewe tu ndiyo unaonekana kung’ara na una nafasi kubwa ya kutoboa kwenye muziki.
Ulikazia kile walichosema kuwa unashukuru Mungu kwa sababu umekuwa ukiongozana na baadhi ya mastaa wakubwa kwenye shoo zao za mikoani, hilo linajidhihirisha kwako kuwa nyota njema imeonekana asubuhi.
Kwa nini rafiki yangu usitumie nyota iliyong’ara kuing’arisha zaidi kuliko kupigania kufifisha bila kujua kama unaififisha?





Amber nakupenda ndiyo maana nakwambia lakini kwa kuwa umeshavurugwa na ukakubali kuvurugika si rahisi kunielewa lakini naamini siku zijazo utanilewa tu.
Kama kaka na rafiki yako nakushauri, kaa chini ujitafakari upya, achana na maisha ya mtandaoni, fanya muziki, jikite zaidi kwenye kuimba, unaweza rafiki yangu au unasubiri hadi msemo wa kusikia kwa kenge atokwe damu masikioni?


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Na.M&U

Read More
      edit
Published 5/18/2017 12:45:00 PM by

MAGAZETI YA LEO MAY 18, 2017









Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Na.M&U



Read More
      edit