Monday, May 8, 2017

Published 5/08/2017 09:04:00 AM by

MAGAZEYI YA LEO MAY 8, 2017








Kwa Ushauri Wa Uhusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Na.M&U
Read More
      edit

Saturday, May 6, 2017

Published 5/06/2017 04:51:00 PM by

WANAWAKE KUKOSA MSISIMKO KATIKA TENDO LA NDOA




WANAWAKE wengi wanasumbuliwa na tatizo la kukosa msisimko lakini kwa bahati mbaya, ni wachache wanaofahamu tatizo linalowasumbua ni nini. Kwa kifupi, hii ni hali ambayo mwanamke anakosa kabisa msisimko na raha ya tendo la ndoa.
Dalili za awali za tatizo hili, ni kama ifuatavyo:
-Kulifikiria tendo la ndoa mara chache zaidi (mwanamke hafikirii mara kwa mara kuhusu tendo la ndoa).
-Kutosikia raha yoyote, kabla, wakati wa tendo au baada ya tendo. Yawezekana mwanamke akawa hasikii maumivu yoyote lakini pia anakuwa hahisi tofauti yoyote.
-Mwanamke kuanza kukataa kushiriki tendo, yawezekana awali alikuwa akikutana na mwenzi wake mara kwa mara lakini ghafla ratiba zinabadilika na hahisi tofauti yoyote.
-Kupoteza kabisa msisimko wa mapenzi. Inapofikia hatua hii, hata kama mwanamke atawekwa kwenye hali ambayo ni rahisi kupata hisia, hushindwa kufanya hivyo.
Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, na sababu hizo zinawekwa katika makundi mawili, za kimaumbile na za kisaikolojia.
Tafiti za kitaalamu, zinaonesha kwamba matatizo ya kisaikolojia huanza hasa baada ya mwanamke kuvunja ungo ambapo mwili huanza kuzalisha homoni ambazo huubadilisha mwili kimuonekano na kihisia.
Homoni hizi zinapozalishwa kwa kiwango kinachostahili, humfanya mwanamke awe na hisia za kawaida kama watu wengine lakini kunapotokea athari yoyote katika uzalishwaji wa homoni hizi, hapo ndipo tatizo huanzia.
Wanawake waliopitia unyanyasaji wa kijinsia wakiwa wadogo, pengine kwa kubakwa, kuteswa kingono, kuteswa kihisia au kunyanyaswa, nao wapo kwenye hatari kubwa ya kupatwa na tatizo hili ukubwani.

Matatizo ya msongo wa mawazo, kusalitiwa kwenye uhusiano wa kimapenzi, kunyanyaswa na mume na uchovu wa kupitiliza (fatigue), husababisha tatizo hili. Kutazama picha za ngono kwa kiwango cha kupitiliza ni tatizo lingine.

Ushauri wangu kwa wapenzi ni vyema mkawa mnashirikishana katika kutimiza ndoto zenu hiii itasaidia inawezekana wewe mpenzi au mkeo unamuona bogaz nyumbani lakini ofisini kwake ni kichwa ni mwanamke ambaye anategemewa katika maamuzi ya kampuni, mtumie na nyumbani ili muanzishe kampuni yenu.
Kwa Ushauri Wa Uhusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Na.M&U

CHANZO: GPL

Read More
      edit
Published 5/06/2017 04:43:00 PM by

KWA NINI UKATISHWE TAMAA NA MWENYE KUKATA TAMAA!


Kwanza napenda kumshukuru Mungu kwa kila jambo katika maisha yangu ya kila siku, najua yapo mengi sana ambayo namkosea. Kwa maneno, matendo na hata kwa kushindwa kutimiza wajibu.

Lakini kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwingi wa rehema bado naipa nafasi ya kuweza kuzungumza na wewe. Tutende mema ndugu zangu. Nikukaribishe kwenye somo la ujasiriamali linalosema:KWA NINI UKATISHWE TAMAA NA MWENYE KUKATA TAMAA!

Ugumu wa maisha anao kila mtu kulinga na uzito wake, kuna wengine wana hali ngumu zaidi lakini kuna wale wenye ahueni.
Katika mafanikio yoyote yale yana changamoto nyingi zipo za mazingira, mtaji, ushauri au watu wanaokuzunguka.

MAZINGIRA
Maeneo uliyopo yanaweza kuwa kigezo cha kukukatisha tamaa kwa namna moja au nyingine katika kufikia jambo fulani. Mazingira unayoishi ni magumu kufanya kile unachokita. Inawezekana umejaribu kila namna lakini bado ikashindikana basi ni vyema ukahama hilo eneo la kwenda eneo ambalo unahisi litakuwa mafanikio kwa kile unachokitaka. Angalizo wakati mwingine ni vyema ukatafuta fursa kulingana na eneo lako.

WATU
Wapo watu wengine wana maono au ndoto nzuri lakini zinashindwa kufanikiwa kwa sababu wanakatishwa tamaa na watu ambao walishakata tamaa zamani kwenye mioyo yao.
Watu wanaoweza kukukatisha tamaa anaweza kuwa ndugu, rafiki au mpenzi wako. Ni vyema wakati unataka ushauri ukachagua mtu au watu wa kukushauri kuliko kuomba ushauri kwa mtu yeyote.

MPENZI
Inawezekana una mpenzi ambaye anakukatisha tamaa kwa sababu wewe una tatizo fulani katika mwili wako labda pengine una ulemavu wa kitu fulani, huna elimu, huna pesa, huna kitu chochote cha maana.

Usikubali kumpa nafasi mtu ambaye ameishakata tamaa siku nyingi, mtu ambaye ana amini kuwa mafanikio yako kwa baadhi ya watu.
Hupaswi kukatishwa tamaa na mwanadamu ambaye ana mapungufu kama wewe, anaumwa kama wewe, analala kama wewe, anahangaika kama wewe, anaugua kama wewe, anakata tamaa kama wewe, alifeli masomo kama wewe, hana kitu kama wewe, siku moja atakufa kama wewe.

Binadamu wengine unaweza kusema labda wamezaliwa kuja kuwamatisha tamaa wenzao yani kila jambo ukifanya umekosea, kila kitu ukisema ni kibaya, wewe mtu wa aina gani, hakuna jema kwako.

Mtu wa namna hiyo ni yule ambaye amefeli katika kufikiria, upeo wake umegota sehemu aamini kama unaweza kuleta maajabu kwa umaskini ulio nao, kwa elimu ndoto uliyonayo, kwa ushamba ulionao. Pigania ndoto zako, acha kusikiliza maneno ya watu ukitaka kuamini kuwa hawafai, wewe acha kutimiza ndoto zako usikie watakavyokusimanga lakini hakikisha umefikia uone kama hawajakusifia kiaina.

Ushauri wangu kwa wapenzi ni vyema mkawa mnashirikishana katika kutimiza ndoto zenu hiii itasaidia inawezekana wewe mpenzi au mkeo unamuona bogaz nyumbani lakini ofisini kwake ni kichwa ni mwanamke ambaye anategemewa katika maamuzi ya kampuni, mtumie na nyumbani ili muanzishe kampuni yenu.
Kwa Ushauri Wa Uhusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Na.M&U


Read More
      edit
Published 5/06/2017 04:23:00 PM by

ANAFAA KUWA MUME AU AUANTAFUTA TU VITU VYANGU?


Mimi ni mwanamke ambaye nafanya kazi kwenye deport ya vinywaji, nimekuwa kwenye uhusiano na kijamana mmoja ambaye tumeanzisha uhusiano kwa muda wa miezi miwili lakini naona kama naumia sana.

Kwani mwenzangu tuliahidiana kuwa mke na mume lakini mwenzangu simuelewi kabisa ni kama haeleweki pamoja na kumpenda, kumjali kumsaidia lakini naona kama siyo mkweli kwangu.

Nimekuwa nikimsaidia sana lakini haoneshi kama ana mapenzi na dhati kwangu kuna wakati Napata hasira na kumdai vitu vyangu.
Naombeni ushauri wenu, anafaa kweli kuwa mume wangu au anatumia tu pesa zangu?.

Kwa Ushauri Wa Uhusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa


Read More
      edit
Published 5/06/2017 02:07:00 PM by

CHANGAMOTO KUBWA INAYOUA BIASHARA


Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na mwamko mkubwa sana wa watu kuingia kwenye biashara. Hii imetokana na hali ya uchumi kuwa ngumu na kipato kimoja, hasa cha mshahara kutokutosheleza mahitaji ya msingi ya maisha. Pia kumekuwa na fursa nyingi za mahitaji ya watu na hivyo watu kuchukua nafasi kutimiza mahitaji hayo na wao kujipatia faida.

Kumekuwa na watu wengi ambao wanafungua biashara ndogo za uchuuzi, na wengine uzalishaji wa bidhaa za vyakula na mavazi. Wapo pia ambao wameingia kwenye kilimo cha kibiashara, na kulima mazao ya matunda na bustani, ambayo yanachukua muda mfupi kulimwa na pia yana uhitaji mkubwa. Fursa zote hizi zimetoa nafasi kwa watu kujiongezea kipato kupitia biashara.






Licha ya kuwepo kwa fursa hizi nzuri za uhitaji wa watu, na licha ya wengi kuingia kwenye biashara hizi, kumekuwa na changamoto moja kubwa sana ambayo imekuwa inaua biashara nyingi ndogo zinazoanzishwa. Tumekuwa tunaona watu wengi wanaanzisha biashara zao wakiwa na hamasa kubwa ya kufanya vizuri, lakini haipiti miezi sita biashara hiyo inakuwa imefungwa. Tunaona watu wanakwenda shambani wakiwa na hamasa kubwa ya kupata faida kwenye kilimo wanachokwenda kufanya, lakini inapofikia wakati wa kuvuna, uzalishaji unakuwa mdogo tofauti na mategemeo, au bei ya soko inakuwa ndogo kuliko gharama mtu alizoingia.

Biashara nyingi zimekuwa zikipata hasara na kupelekea kufungwa kutokana na changamoto hii ambayo inawakumba wafanyabiashara wengi. Leo kupitia makala hii tutakwenda kuichambua changamoto hii kwa kina, ili uweze kuondoka na kitu cha kufanyia kazi, na unapoanzisha au kukuza biashara uliyonayo sasa, usiingie kwenye makosa ambayo umekuwa unafanya miaka yote.

Changamoto ambayo imekuwa inaua biashara nyingi ndogo hapa Tanzania, ni namna ya kufikiri ambayo wafanyabiashara wanayo. Watu wengi wanaingia kwenye biashara wakiwa hawana taarifa kamili. Wanaingia kwenye biashara wakiwa na taarifa za upande mmoja pekee wa biashara, na hivyo kupata shida pale wanapokutana na changamoto za upande mwingine wa biashara. Kwa kifupi, watu wengi wanaingia kwenye biashara wakiwa na wazo moja tu, nikizalisha watu watanunua, au nikiuza, watu watakuja kununua. Hii ni mbinu ambayo ilikuwa na mafanikio zamani, wakati wachache ndiyo walikuwa wanafanya biashara, ila kwa sasa karibu kila mtu anafanya biashara, unahitaji mbinu za ziada ili kuweza kuikuza biashara yako.

Watu wengi wamekuwa wakiingia kwenye biashara baada ya kuona wengine wanafanya, na kwa kuwa wanaona watu hao wanafanya na wana wateja, basi moja kwa moja wanahitimisha kwamba biashara hii ina wateja wengi na inalipa, wacha na mimi niingie kwenye biashara hii. Wengine wamekuwa wanaingia kwenye biashara baada ya kusikia watu wanasema biashara hiyo inalipa, wanahamasika kupitia maneno wanayosikia, na kujikuta wameshaingia kwenye biashara ambayo hawakuijua vizuri. Kwa kuangalia kwa nje, kila biashara inalipa, kwenye hesabu za makaratasi, kila biashara inalipa. Nimekuwa nawaambia watu, sijawahi kuona mchanganuo wa biashara ambao una hasara, lakini karibu kila biashara ina hasara. Kwa kuangalia upande huu mmoja wa biashara, wafanyabiashara wengi wamekuwa wakiingia kwenye biashara na kujikuta kwenye wakati mgumu.

Hapa nakushirikisha mambo matatu muhimu ya kuzingatia kabla hujaamua kuingia kwenye biashara yoyote ile, iwe ni kuuza bidhaa, huduma au kufanya kilimo cha kibiashara.

Moja; fanya utafiti wa biashara kabla hujaingia kwenye biashara hiyo. Usiingie kwenye biashara kwa sababu unaona watu wanafanya na wana wateja, au kwa sababu umesikia kila mtu anaimba kilimo fulani kinalipa. Jipe muda na fanya utafiti, na utafiti huu ninaokuambia ufanye siyo wa kwenda kutafuta na kusoma kwenye mtandao au vitabu, badala yake watembelee wale wanaofanya biashara hiyo. Fanya nao urafiki na jifunze mengi kutoka kwao, namna wanavyo endesha biashara zao, changamoto wanazokutana nazo, na hata wanavyozitatua. Pia fanya utafiti kwa wateja wa biashara hiyo, wanapatikana wapi, mahitaji yao ni yapi na uwezo wao wa kumudu gharama za biashara husika.

Mbili; ifikirie biashara kwa ujumla, ifikirie kama mfumo na siyo kama kitu kimoja. Biashara yoyote, kwa kiwango cha chini kabisa inahitaji kuwa na angalau mifumo mitatu, usimamizi, uzalishaji na masoko/uuzaji. Wengi wanaoingia kwenye biashara huwa wanafikiria uzalishaji pekee, usimamizi na masoko/uuzaji huwa wanafikiri ni vitu vinavyokuja vyenyewe pale biashara inapokuwa imeshaanza. Matokeo yake ni watu wengi kuingia kwenye biashara na baadaye kukosa soko. Unapoingia kwenye biashara, jua kwa kina kuhusu usimamizi wa biashara hiyo, unachozalisha na soko lako na namna unavyolifikia soko hilo.


Tatu; jitofautishe na wafanyabiashara wengine. Japo kwa sehemu kubwa wazo lako la biashara utakuwa umelipata kutoka kwenye mawazo ya wengine, usifungue biashara inayofanana na wengine kwa kila kitu. Tafuta njia ya kujitofautisha, hata kama biashara mnayofanya inafanana. Lazima uwe na kitu ambacho wateja wanakipata kwako tu na siyo kwa wengine. Kama biashara zinafanana, basi toa huduma bora zaidi ya wanazotoa wengine. Mteja anapokuwa kwenye biashara yako, ajisikie tofauti kabisa na akienda kwenye biashara nyingine. Njoo na mbinu tofauti za ufanyaji wa biashara yako, kama wengine wanasubiri wateja waje kwenye biashara zao, wewe unaweza kuwafuata wateja kule walipo.

Ni hatari sana kuingia kwenye biashara ambayo hujaijua vizuri, hakikisha umefanya utafiti, kujua biashara nzima na kujitofautisha na wengine. Kwa kufanya hivi utaondokana na changamoto inayoua biashara nyingi. Kila la kheri. 


Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     


Read More
      edit
Published 5/06/2017 08:48:00 AM by

MAGAZET YA LEO MAY 6, 2017











Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     

Read More
      edit

Friday, May 5, 2017

Published 5/05/2017 10:03:00 PM by

HAKUNA MWANAUME ANAYELIDHIKA NA MWANAMKE MMOJA




Mtangazaji na Mchoraji katuni maarufu nchini Tanzania,Masoud Kipanya amewaaacha watanzania midomo wazi kwa kuweka wazi maoni yake kuwa mwanaume hawezi kuridhika na mwanamke mmoja.
Masoud amesema tangia zamani wanaume ni Watu mwenye tamaa hivyo hakuna mwanaume ambae anapenda kuwa na mwanamke mmoja ila ni vitu vidogo vidogo tu vinavyozuia kama dini ya Kikristo na masuala mengine ya kiuchumi.

“Hakuna mwanaume anaependa kuwa na mwanamke mmoja,na hiyo ndiyo huruka ya uanaume,tunajizuia tu kwa sababu!! hivyo kwa mfano kwa wenzangu wakristo utaratibu unawazuia lakini angalia vidumu vilivyo nje unaona eeehh??“

Amesema Masoud Kipanya kwenye Mahojiano yake na Kwanza TV.
Hata hivyo Masoud alizungumzia suala la idadi ya kuzaa watoto kwenye familia na kusema kuwa kwa upande wake  yeye hana kikomo kwenye kuzaa kwani anaamini watoto hawarishwi na yeye bali wanarishwa na mwenyezi Mungu.
Masoud Kipanya kwa mujibu wa Takwimu za mwaka jana zilizofanywa na kituo cha Clouds FM kupitia kipindi cha XXl ni moja ya watu watatu maarufu nchini Tanzania wanaoendesha magari ya kifahari akiwa anamiliki gari aina ya Hummer H3.


Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     

Read More
      edit
Published 5/05/2017 06:19:00 PM by

MBINU BORA ZA KUMRUDISHA THAMANI YA MWENZI WAKO KATIKA MAISHA


Ni wazi kwamba hakuna wito wowote duniani ambao hauna changamoto, kumbe basi kila wito ambao umeuchangua kuuishi tarajia kukutana na changamoto na wala usijidanganye kuwa wito Fulani ndiyo bora kwani hakuna familia iliyokuwa salama kwa kila kitu. Baada ya wanandoa kufunga ndoa huwa wanakua na maisha ya furaha na amani siku za mwanzo ila kadiri siku zinavyokwenda kila mmoja anaanza kupoteza thamani ya mwenzake taratibu.


Pale mtu anapoamua kufunga ndoa kwa hiyari yake yeye mwenye anakuwa na shauku na hamasa ya kumfurahia mwenzake kuishi naye pamoja na kutambua thamani ya mwenzake. 

Baada ya wanandoa kutarajia kupata kitu Fulani kutoka kwa mwenza wake na kukosa kile alichotarajia kukipata basi anaanza kupoteza ladha au thamani kwa mwenza wake. Mwanzo kila mmoja anakuwa kama chumvi yenye ladha katika chakula lakini baadaye mmoja wa wanandoa anaweza kuwa chumvi iliyokosa thamani katika mahusiano yao.

Kama tunavyojua rafiki, kazi ya chumvi ni kuleta ladha katika chakula je kama wewe uko katika mahusiano ya ndoa na mwenzako ukishamuona kama chumvi iliyokosa thamani, yaani iliyopoteza ladha huwezi kumfurahia hili tunaweza kuliona hata katika mfano wa chakula kilichokosa chumvi huwa hakina ladha kabisa na unakuwa huna hamasa ya kukila chakula hicho.

Kila mmoja huenda amepoteza ladha kwa mwenzake pengine kwa kushindwa kumtimizia mwenzake haja yake au njaa yake. Kama tunavyojua wanandoa ambao ni mwanamke na mwanaume wote hawa kila mmoja ana njaa yake hivyo ukishindwa kushibisha njaa ya mwenzako unakuwa umepoteza ladha au thamani hivyo unakuwa kama chumvi iliyopoteza ladha.


Mwanamke na mwanaume ni viumbe viwili ambavyo kila mmoja anatoka katika sayari yake. Wanaume wanatokea katika sayari ya mars na wanawake nao wanatokea katika sayari ya venas. Kutokea katika sayari tofauti maana yake hawafanani na wako tofauti, 
Mbinu itakayoweza kurudisha thamani katika mahusiano yako ni mbinu ya negative visualization yaani taswira hasi. Hii ni mbinu ya wanafalsafa wa ustoa yaani stoic philosophy iliyotumiwa na wanafalsafa wa zamani kama vile zeno, Seneca kabla hata ya Yesu kuzaliwa kuishi maisha bora yenye furaha na mafanikio makubwa .

Rafiki, kujenga taswira hasi kwa mwenzi wako wa ndoa itakusaidia kurudisha ladha au upendo uliopotea kwa mfano kama unahisi mwenzi wako amepoteza thamani kwako anza kumjengea taswira hasi jenga picha akili kabisa tayari ameshakufa kwa sababu kila ulichonacho hapo sasa umepewa kwa muda tu utaviacha tu. Kama umevuta taswira hasi mwenzi uliyekuwa naye ndiyo hayupo tena na hapo mwanzo alikuwa na thamani kubwa basi ndiyo utaanza kuona thamani yake.


Jenga taswira hasi kuwa mwezi uliye naye sasa hivi kesho siyo wako utanyang’anywa kwa hiyo, kama ulikuwa haumpi thamani utaanza kumthamini huku ukijua kuwa utanyang’anywa muda wote wote kwa hiyo, lazima utampa thamani ya hali juu sana. Hata asubuhi unavyomuaga mwezi wako jenga taswira kuwa kama ndiyo mara yako ya mwisho kuonana naye kwa hiyo unatakiwa kumwaga kwa thamani na kumtumia vizuri kwa muda huo ambao upo naye. Wazungu wanasema never take any things for granted yaani usichukulie kitu chochote kama kipo tu au umepewa kirahisi, kama una mke , mume wako mtumie vizuri sasa kipindi yuko hai hata siku akifa hutojutia kuliko kumchukulia yupo tu kila siku na huoni thamani yake.

Unaweza kuitumia mbinu hii katika mahusiano yoyote yale uliyonayo kama una mama yako yuko hai basi mtumie vizuri kabla hajaondoka kwani kila uliye naye sasa hivi umeazimwa kwa muda. Ni sheria ya asili kuwa hakuna mtu atakayeishi milele, na hakuna mtu ambaye ana mkataba wa kudumu wa kuishi milele na yule aliye naye sasa. Kama uko katika ndoa basi kila mmoja anatakiwa kujiandaa kisaikolojia kuwa yeye ni mjane mtarajiwa. Kama unamuaga rafiki yako basi muage vizuri` na kuamini kuwa hiyo ndiyo siku yako ya mwisho kuonana naye.


K ama umejenga taswira hasi kwa mwenzi wako hutoweza kumchukulia kirahisi hata kama ana mapungufu kiasi gani lazima utatumia vizuri uwepo wake. Ishi na mwenzi wako huku kila mmoja akimtumia mwenzake vizuri na kutumia thamani yake vema huku akiamini kuwa muda huo ambao mko sasa ndiyo muda wenu wa mwisho kuwa pamoja. Kama unambusu na kumkumbatia mtoto wako, mwenzi wako basi mbusu kwa thamani kubwa huku ukiamini kuwa ndiyo mara yako ya mwisho kumfanyia vitu hivyo. 

Lazima kujitoa kwa moyo na kutambua thamani ya mwenzako kama ukimjenga taswira hasi ya kuwa uko naye hapo kwa muda tu hivyo unatakiwa kumtumia vizuri kabla hajaondoka.




Hatua ya kuchukua, tumia mbinu hii ya negative visualization yaani taswira hasi kurudisha amani, upendo, furaha , thamani katika maisha yako ya ndoa na mahusiano yako na watu wengine. usimchukulie huyo uliye naye sasa hivi yupo tu kimazoea bali mchukulie wa thamani kubwa kwamba unanyang’anywa muda wote wote ule ni sawa sawa na ukiambiwa kuwa umeme utakatika baada ya dakika chache na utarudi baada ya wiki mbili hakika kama una nguo za kunyoosha lazima utanyoosha haraka tena za wiki nzima hutoweza kuuchukulia tena upo kwani tayari umeshaambiwa hautokuwepo tena hivyo lazima utautumia vizuri kabisa.

Mwisho, kila mtu ana udhaifu wake na thamani yake hivyo tumia vizuri thamani yake kwa kipindi ambacho uko naye sasa ili hata akiondoka hutoweza kujutia kwa sababu ulimtumia vizuri. Chochote unachomfanyia mwenzi wako jenga taswira hasi kuwa ndiyo siku ya mwisho kumfanyia kitu au jambo hilo hivyo huwezi kufanya kimakosa utahakikisha unajitoa kwa moyo wote. Usitafute ubaya kwa mwenzako kwani ukitafuta ubaya tarajia tu kuupata.

Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     
Read More
      edit
Published 5/05/2017 05:29:00 PM by

BABY MADAHA ADAIWA KUHONGWA GARI

MSANII wa muziki na filamu Bongo, Baby Madaha amegandwa na skendo ya kuhongwa gari kisha baadaye kupokonywa na aliyekuwa meneja wake, Joe Kairuki, Ijumaa limevujishiwa hii ‘untold story’.
Ilidaiwa kuwa, kipindi cha nyuma wakati Madaha akiwa Kenya chini ya Lebo ya Candy ‘n’ Candy ya Joe, wawili hao walianzisha uhusiano wa kimapenzi ndipo mwanadada huyo akapewa ndinga hiyo aina ya Audi ya kuuzia sura.
Baada ya Madaha kupewa gari hilo, alijinadi kuwa, amepewa ikiwa ni sehemu ya mkataba wake lakini wanaoujua mchezo mzima wakavujisha ubuyu kuwa, alihongwa na baadaye akapokonywa.




Katika kuashiria kuwa madai ya kuhongwa yana ukweli f’lani ndani yake, baada ya Madaha kuachana na jamaa huyo, gari nayo akapokonywa na aliporudi Dar hakuwa na usafiri. Kufuatia madai hayo kusambaa kwa muda mrefu, hivi karibuni gazeti hili lilizungumza na Madaha na alipobanwa kuwa lile gari halikuwa lake bali alihongwa kisha akapokonywa alisema: “Hao wanaosema nilihongwa wana ushahidi gani? Ile gari nilipewa kama sehemu ya mkataba wangu, nilipomalizana nao nikaona nisije nayo Dar, nikaiuza.
Ijumaa: Ubuyu uliopo ni kwamba, Joe alikuwa mpenzi wako ndiyo maana akakupa ile gari, mlivyozinguana akachukua gari yake.
Madaha: Kwanza Joe hakuwahi kuwa mpenzi wangu jamani.
Ijumaa: Sasa wewe unasema uliiuza, mbona inadaiwa Joe ndiye anayeitumia kwa sasa?

Madaha: Niliyemuuzia ni rafiki yake aliyekuwa Mombasa, sasa kama imemrudia tena sijui imekuwaje.

Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     
Read More
      edit
Published 5/05/2017 09:11:00 AM by

MAGAZETI YA LEO MAY 5, 2017










Kwa ushauri wa mahusiano, hadithi za mapenzi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali.

Jiunge na M&U WhatsApp na M&U SMS kupitia 0679979785 au tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwenye Mtandao wa Kijamii wa Facebook.
Na:M&U     
Read More
      edit