Wednesday, July 12, 2017

Published 7/12/2017 06:01:00 PM by with 0 comment

SAFARI YA MWISHO YA MTANGAZAJI WA REDIO 93.7 EFM, SETH KATENDE MAARUFU BIKIRA WA KISUKUMA


Jeneza lenye mwili wa Marehemu Seth Katende maarufu kama Bikira wa Kisukuma ambaye alikuwa Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha 93.7 EFM kupitia kipindi cha Ubaoni, likiwa katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam kunakofanyika misa ya kuaga mwili wake hivi sasa, ambapo baada ya kumalizika kwa misa hiyo, Mwili wa Marehemu utapumzishwa kwenye nyumba yake ya Milele katika Makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es salaam mchana wa leo.

Sehemu ya Waombolezaji wakiwa katika Viwanja Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam kunakofanyika misa ya kuaga mwili wake hivi sasa, ambapo baada ya kumalizika kwa misa hiyo, Mwili wa Marehemu utapumzishwa kwenye nyumba yake ya Milele katika Makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es salaam mchana wa leo.


Read More
      edit

Tuesday, July 11, 2017

Published 7/11/2017 10:56:00 AM by

NIACHE MASOMO ILI NIFANYE BIASHARA


Nina mke na mtoto mmoja. Kwa sasa nimeajiriwa kama mhasibu msaidizi katika kampuni moja hapa Dar es Salaam. Mwaka mmoja baada ya ajira niliamua kujiunga na masomo ya CPA ili kuongeza thamani ya taaluma yangu ya uhasibu. Changamoto yangu kipato hakitoshi masomo magumu na yanachukua muda zaidi kutokana muda mwingi kuwa ofisini. Hivyo nafikiria kuachana na masomo na hiyo fedha ambayo naiwekeza kwenye masomo ya CPA nafikiria niiwekeze kwenye biashara ingawa natamani kuendelea na masomo ya CPA. Naomba ushauri maana naona umri unazidi kwenda (nina miaka 33) niachane na CPA na kutafuta biashara ya kufanya na kuweka juhudi zaidi huko? Ahsnte – 

Pole sana kwa changamoto hiyo unayopitia. Ni wakati mgumu sana uliopo, kama umeajiriwa, una familia, kipato kidogo na kama hayo hayatoshi, una masomo magumu ambayo pia yanakugharimu.
Ni wakati mgumu sana, lakini kabla ya kufanya maamuzi yoyote, lazima ukae chini na kutafakari kwa makini maisha yako na ndoto zako kubwa, yapi maono ya maisha yako, kupanga vipaumbele vyako vizuri na kisha kuweka mkakati ambao utaufanyia kazi, kwa nidhamu ya hali ya juu sana.
Hivyo, kabla hujafanyia kazi ushauri ambao nitakupa hapa, kaa chini kwanza uangalie maisha yako na maono yako. Kisha angalia hatua mbayo utaichukua.
Baada ya hayo, ushauri wangu ninaokupa ni huu; FANYA VYOTE KWA PAMOJA.
Ndiyo, namaanisha ufanye vitu vyote hivyo kwa pamoja. Yaani una familia, umeajiriwa, una masomo na unafikiria kuhusu biashara. Badala ya kutaka kuacha masomo ili ufanye biashara, fanya masomo na fanya biashara. Huenda hukutegemea jibu hili na huenda una wasiwasi haiwezekani, lakini nakuambia inawezekana kama kweli utaamua liwezekane.
Nina amini masomo yako ya CPA hayatachukua zaidi ya miaka mitatu, hivyo basi rafiki, nataka ujitangazie miaka mitatu ya vita. Hii inakwenda kuwa miaka mitatu ya tofauti kabisa kwenye maisha yako, miaka mitatu ya kuyajenga upya maisha yako.
Kwenye miaka hii mitatu, jipe ruhusa kabisa ya kwenda kinyume na maisha yote ya kijamii, kwa sababu jukumu lililopo mbele yako siyo dogo, ni kubwa sana, hivyo linakuhitaji na wewe uwe na maamuzi ambayo wengine hawatakuelewa.
Kwa uzoefu wangu binafsi na kupitia watu ambao nimewashauri, nimekuja kugundua karibu kila mmoja wetu ana uzembe fulani ambao unamrudisha nyuma. Licha kweli ya maisha kuwa magumu, kipato kidogo na kazi kuwa nyingi, bado tuna uzembe ambao tunaufanya, na uzembe huu unaturudisha nyuma.
Kwa mfano, utakuta mtu pamoja na changamoto alizonazo, bado anapata muda wa kuangalia tv, kusoma magazeti, kusikiliza redio. Bado ana muda wa kufuatilia mpira, anakaa kabisa chini dakika 90 kuangalia mpira. Bado ana marafiki anaokutana nao jioni na wanakaa kupiga stori, labda wakipata vinywaji. Mtu huyu huyu yupo kwenye mitandao ya kijamii, analala muda wa zaidi ya masaa sita. Mtu huyo unakuta siku za kazi ni tano, jumatatu mpaka ijumaa, na jumamosi labda nusu siku, halafu jumapili anapumzika. Mtu huyo huyo ana mambo mengi ambayo yanampotezea fedha lakini hakuna hatua anazochukua. Na mambo yanapokwenda hivi, lazima maisha yazidi kuwa magumu.
Hivyo hatua za kuchukua ni hizi;
  1. Badili kabisa mfumo wako wa maisha.
Tenga miaka hiyo mitatu kama nilivyokueleza hapo juu, miaka hiyo hakikisha unaimaliza cpa, unaongeza kipato chako kupitia biashara, na kuimarisha maisha yako.
Weka thamani kubwa sana kwenye muda wako, usipoteze hata dakika yako moja. Punguza watu na mambo mengine yoyote ambayo siyo muhimu kwako. Kama kuna mtu ambaye hatakuelewa kwa mabadiliko ya maisha utakayofanya, siyo muhimu, achana naye. Kaa na wale watu wanaoelewa unakoenda, na wanakuunga mkono na kukusaidia. Achana na watakaokukatisha tamaa, na kwa taarifa tu, watakuwa wengi.
  1. Chagua biashara ambayo utaifanya.
Chagua biashara ambayo unaweza kuifanya, kwa kuanzia hapo ulipo sasa. Na kwa kuwa muda wako ni mdogo, nakushauri uanzishe biashara ya huduma, ambapo utatoa ulichonacho kwa wengine.
Kwa mfano wewe umesema ni mhasibu, sasa angalia unawezaje kutumia uhasibu wako kama huduma na kuiuza kwa wengine.
Je unaweza kuwasaidia wafanyabiashara wadogo na wa kati kuandaa mahesabu ya biashara zao?
Je unaweza kupata kazi ya muda wa ziada kazini kwako au sehemu nyingine ambayo unaweza kutoa thamani zaidi?
Je unaweza kutoa huduma ya kuwafundisha watu wengine wanaojifunza uhasibu au kitu kingine ambacho unaweza kufundisha?
Je unaweza kuanzisha biashara nyingine ndogo ukapata mtu wa kuifanya kwa karibu na wewe ukapata muda wa kuifuatilia kila siku?
Endelea kujiuliza maswali hayo, kulingana na mazingira yako mpaka upate jibu lenye kuweza kufanyika. Lazima upate jibu na kuanza kulifanyia kazi mapema.
  1. Panga ratiba ya kila siku ambayo utaisimamia vizuri.
Kitu muhimu sana ambacho unapaswa kufanya, ni kupangilia ratiba yako ya kila siku. Na anza na mpango wa siku ambao una mambo utakayoyafanya kila siku. Kwa mfano kwako wewe, kazi, masomo, biashara na familia ni mambo ambayo lazima uyafanye kila siku.
Hivyo hakikisha kila siku ya kazi, unatenga muda ambao utakuwa wa kufanya kazi.
Katika siku nyingine zote za wiki, panga muda wa kusoma masomo yako, na pia panga muda wa kufanya kazi kwenye biashara yako. Hili ni kila siku, kumbuka kwa sasa huna siku ya mapumziko, utaendesha maisha yako siku saba za wiki, na siku ambayo huendi kazini ndiyo unazitumia vizuri zaidi.
Panga kuamka mapema kuliko ulivyozoea, aka masaa mawili au hata moja kabla ya muda wako wa kawaida wa kuamka. Na muda huo utumie kusoma, kila siku. Unapokuwa kazini, muda wowote unaopata wa mapumziko, usiupoteze, badala yake utumie kusoma. Jioni ukitoka kazini, usipoteze muda, weka muda huo kwenye biashara yako.
Kusoma na biashara vikweke kwenye ratiba yako ya kila siku. Najua watu wengi huwa hawasomi mpaka mitihani ikaribie, wewe usiwe mtu wa aina hii. Kuanzia siku ya kwanza unapojiandikisha na masomo na kupata mtaala, panga ratiba ya kila siku utasoma nini mpaka unapofikia wakati wa mtihani. Kwa njia hii utakuwa na maandalizi mazuri na mambo yako mengine yataenda. Kama ukiweza kujijengea nidhamu, unaweza kuweka muda wako kwenye kujisomea mwenyewe na kuepuka kuhudhuria madarasa ambayo yatakuhitaji kulipa fedha zaidi.
  1. Jenga nidhamu ya hali ya juu sana, mambo hayatakuwa rahisi.
Kusoma hapa itakuwa rahisi, na unaweza ukaona eh, nitafanya hivi. Lakini siku ya kwanza kuanza kufanya tu, dunia yote itakupinga. Utafika wakati wa kuamka na utajiambia kwa nini niamke leo, nitaamka kesho. Utafika kazini na kupewa majukumu zaidi. Utapanga ratiba ya kusoma na kuona mtihani bado upo mbali, utasoma tu.
Dunia inakusubiri ikuangushe, hivyo jiandae vizuri sana, tena sana. Na usikubali kwa namna yoyote ile kuvunja kile ulichopanga. Kwa lolote linalotokea ambalo hukutegemea, jipange kuhakikisha mambo yako yanaenda kama ulivyopanga.

Jambo moja naweza kukuhakikishia ni kwamba, maisha yatakuwa magumu, lakini kwa uhakika zaidi ni kwamba hutakufa, utazidi kuwa imara na maisha yako yatakuwa bora zaidi.
Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Na.Mi&u

Read More
      edit
Published 7/11/2017 10:01:00 AM by

MAGAZETI YA LEO JULY 11, 2017






Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Na.Mi&u

CHANZO: GPL
Read More
      edit

Sunday, July 9, 2017

Published 7/09/2017 01:19:00 PM by

PICHA ZA HARUSI YA PROFESA JAY NA MKEWE GRACE










Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa

Na.Mi&u

CHANZO: MILARD AYO
Read More
      edit

Friday, July 7, 2017

Published 7/07/2017 09:41:00 PM by

NAHISI KUJITOA ROHO KISA MKE WANGU AU NIMFANYAJE?




Nina miaka zaidi ya 7 kwenye ndoa ya mke mmoja na watoto watatu ambao wengine ni wakubwa wakiwa ngazi ya sekondari kimasomi.
Kuna wakati ndoa yangu ilikuwa na migogoro ya hapa na pale kwa sana Kiasi kwamba ikafika sehemu mke wangu akatoroka nyumbani kwa kusomba kila kitu wakati mimi nikiwa kwenye mizunguko yangu.


Maisha yaliendelea kwa muda nikiwa pekee yangu lakini baadaye mke wangu alirejea nyumbani. Ila kuna kitu nilikigundua kwake alivyotoroka na alivyorudi kulikuwa na mabadiliko sana, kwanza amekuwa na kibuli na dharau hasa. Nilivumumilia.


Kuna wakati maisha yaliyumba sana kwa upande wangu kwa sababu niliacha kazi niliyokuwa nayo. Kwa kuwa watu mtaani walikuwa wanajua kazi ambazo ninazifanya, mmoja wa jirani yetu akaniambia anipe kazi ya ulinzi kwake, ila bahati nzuri nikawa nimepata kazi kwingine.


Yule mwanaume, mkewe na mke wangu ni marafiki walioshibana sana. Baada ya kuona maisha yetu hayako sawa, yule mama aliongea na mke wangu ili twende tukaishi kwenye nyumba yao iliyoko shamba, tukakubali.
Baada ya muda kupita nikagundua kuwa yule baba mwenye nyumba ninayoishia anatembea na mke wangu. Kumbe siku zote migogoro na mifarakano na mke wangu yeye ndiye hasa aliyekuwa anahusika.


Nimeumia sana, natamani hata nijichome kisu kwa hasira nilizonazo, kumbe jamaa alinipa msaada ili atembee na mke wangu, inaniuma sana. Natamani nichukue maamuzi magumu lakini watoto wangu wananiuma na ninawapenda sana.
Naomba ushauri wako wa mwisho ili nijue nini chakufanya.


Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.

Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Na.Mi&u


Read More
      edit

Monday, July 3, 2017

Published 7/03/2017 12:27:00 PM by

MAGAZETI YA LEO JULY 3, 2017





Kwa Ushauri Wa Mahusiano, Mada Za Mahaba, Hadithi, Machombezo, Mikasa Ya Kweli Ya Mapenzi Na Ujasiriamali. Jiunge na M&U SMS au M&U WhatsApp kupitia Na. 0679979785.


Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
Read More
      edit

Saturday, July 1, 2017

Published 7/01/2017 03:42:00 PM by

ILI UFANIKIWE, LAZIMJA UTESEKA KWA MALENGO


Jumamosi nyingine kwa upendo wa Mungu tunaweza kukutana tena kwa ajili ya kujadiliana kuhusu changamoto mbalimbali maisha na mapenzi. Somo la leo linahusu kujitesa kwa muda ili uweze kufanikiwa katika kutimiza malengo au ndoto zako.

Ndugu yangu mtu yeyote unayemuona  au kumsikia kuwa kafanikwa basi ni lazima atakuwa alijitesa kama siyo yeye basi kuna watu waliteseka kwa ajili yake.Huwezi kufanikiwa kwa hisia, fikra, maneno au kwa kusubiri f’lani akulete au ushushiwe mafanikio unayoyataka.

Si rahisi kufanikiwa kwa kuwa msikini wa kufikiri au mtu ambaye unapenda kuwa tegemezi.Mafanikio yoyote yanahitaji uteseke, ujitume, uthubutu ili kuweza kuyapata au kuyafikia.
Ukitaka kufanikiwa katika jambo fulani ni lazima ukubali kuteseka kwa malengo, kwa mfano unaishi na mtu lakini inaonekana anakunyanyasa basi ni lazima uvumilie yale mateso wakati unatafuta namna ya kuanza kujitegemea, lazima uumize kichwa ni kwa namna gani utaweza kupata kazi ya kukuingizia kipato kitakachokuwezesha kujikimu kwa kulipa kodi, chakula ma mambo mengine.

MATESO YA KUJIAJIRI
Hapa nitajaribu kuzungumza na mtu ambaye anatamani atoke kimaisha lakini anashindwa, yumkini umeajiriwa lakini unaona kabisa una kila sababu ya kujiajiri ila unashindwa, basi lazima uendele kufanya kazi kwa mateso ya mafanikio, endelea kuumia na kuteseka kwa malengo. 
Malengo yako unaweza kuweka ya mwezi mmoja, miezi mitatu, na kuendelea inategemea na ndoto zako. Kwa hiyo unaweza kuchagua mwenyewe uteseka kwa muda gani na kwa ajili ya kupata nini? Unachotakiwa ni wewe kuwa na uchungu na kile ambacho unataka kukifanya au kukikamilisha.

MATESO MENGINE NI YA MATUMIZI 
Kama ulikuwa unatumia Sh.10,000 kwa siku basi punguza anza kutumia 5,000. Kama asubuhi pekee, ulikuwa unakunywa chai ya Sh. 3,000 basi anza kunywa ya 1,500  kwa maana ya kwamba kama ulikuwa unakunywa chain a chapatti 2 au zaidi basi kunywa chai na chapati moja, utumbo utapwaya lakini huwezi kufa kwa kutokula chapati mbili.

Tena chai hiyo unaweza kuivutia muda kidogo angalau saa nne au saa tano ndipo ukanywa ili ikusaidie kukufikisha kwenye chakula cha mchana.
Ukishapiga chai na chapati yako moja amchain a kitafunwa kimoja kisha ukasubiri mchana ndiyo ukala kwa kushiba au unaweza kuipotezea kabisa chai kwa muda wa miezi 3 ili kuangalia kama malengo yako yamefanikiwa. Kuwa na malengo yasiyo kufikirisha na kukuumiza kiakili, kimwili na kimtazamo, hakikisha unajiwekea malengo yenye maumivu ili uweze kufanikiwa lasivyo utaendelea kuwa hivyohivyo siku zote.

Kwa ushauri wa mahusiano, mada za mahaba, hadithi, machombezo, mikasa ya kweli ya mapenzi na ujasiriamali. Jiunge na Mi&u SMS au Mi&u WhatsApp kupitia Na. 0679979785.
Pia tembelea www.miminauhusiano.blogspot.com, Insta:@mimi_na_uhusiano au tembelea ukurasa wetu wa Mimi na Uhusiano kwa ku-Bonyeza Hapa
#Mi&u
Read More
      edit
Published 7/01/2017 03:07:00 PM by

CHANGAMOTO KATIKA BIASHARA


Biashara zina changamoto, lakini pale mfanyabiashara mwenyewe anaongeza changamoto, biashara inakuwa ngumu zaidi. Wafanyabiashara wengi wamekuwa wakitengeneza changamoto nyingi kwenye biashara zao wao wenyewe na hivyo kujizuia wao wenyewe kufanikiwa. Hii ni sawa mtu anaendesha gari, huku amekanyaga mafuta na breki kwa wakati mmoja. Atatumia mafuta ya kutosha lakini hatafika popote.

1.  Kutaka kurahisisha biashara.
Nimekuwa naona wafanyabiashara wengi, hasa wanaoanza wanapojaribu kukwepa kufanya kazi zao. Wengi wamekuwa wanafikiri kwa kumiliki biashara zao, basi hakuna wa kuwapangia wafanye nini na kwa wakati gani. Hivyo hujiona kama mabosi ambao kazi yao ni kuwatuma watu wengine. Kwa njia hii wamekuwa wakijikuta wanapata changamoto nyingi kama za wasaidizi kuharibu biashara, wateja kupata huduma mbovu na hata mzunguko wa fedha kutokuwa mzuri.
Kitu unachopaswa kujua ni kwamba, biashara yako inakutegemea sana wewe, lazima uwe karibu sana na biashara yako, lazima ujue kila kinachoendelea kwenye biashara yako. Na hapo unaweza kuchukua hatua sahihi kabla mambo hayajaharibika zaidi. Usitake kurahisisha biashara, usitafute ubosi wa haraka, endesha biashara yako vizuri, kaa nayo karibu na jua kila kitu.

2. Kuchanganya matumizi ya kawaida na fedha za biashara.
Hii ni changamoto moja kubwa ambayo inaua biashara nyingi ndogo. Kabla hata hatujaenda mbali sana, wewe jaribu tu kuangalia biashara nyingi za nyumbani, labda duka linalofunguliwa nyumbani ambalo ni la mahitaji muhimu. Huwa ni biashara ambazo wengi hawaoni faida. Tena wapo ambao wamekuwa wanafungua na kufunga biashara hizo mara kwa mara.
Kushindwa kutenganisha au kutofautisha matumizi ya kawaida na fedha binafsi, kunawafanya wafanyabiashara kutengeneza changamoto ya mzunguko wa fedha kwenye biashara. Hii ni kwa sababu fedha nyingi inaondoka kwenye biashara na hivyo biashara kushindwa kujiendesha yenyewe.
Unapokuwa kwenye biashara, jua kabisa kwamba wewe na biashara yako ni vitu viwili tofauti kabisa, ndiyo biashara ni yako, lakini siyo wewe. Hivyo mambo ya biashara lazima yawe chini ya biashara, na mambo yako binafsi lazima yawe chini yako. Usichanganye mambo haya, kila kitu kiende kwa kumbukumbu.

3. Kuajiri watu wasio na sifa au uwezo wa kufanya kazi kwenye biashara.
Hii ni changamoto nyingine ambayo wafanyabiashara wenyewe wamekuwa wanaitengeneza. Wafanyabiashara wengi wadogo na wa kati, inapofika wakati wa kuajiri, huangalia watu wanaoweza kuwaajiri na kuwalipa kiasi kidogo cha fedha. Na kama unavyojua, watu ambao wapo tayari kulipwa kiasi kidogo cha fedha, ni watu ambao hawana kitu kingine cha kufanya. Sasa kama mtu hana kitu kingine anaweza kufanya, unafikiri ataweza kuwa wa msaada kwenye biashara yako?
Unapopanga kuajiri wasaidizi kwenye biashara yako, angalia watu wenye sifa zinazoendana na kazi unayopanga kuwapa. Pia wawe na uwezo wa kutekeleza majukumu unayowapangia kufanya. Hata kama huna uwezo wa kuwalipa kiasi kikubwa, kuwapata watu hao unaweza kuona namna gani wanaweza kunufaika zaidi kupitia wewe.


4. Kukopesha wateja bidhaa au huduma.
Hii pia ni changamoto ambayo mfanyabiashara mwenyewe anajitengenezea. Anajikuta akiwapa wateja bidhaa au huduma kwa mkopo, kwa ahadi ya kulipwa baadaye. Lakini kinachotokea ni kwamba baadhi ya wanaokopa wanakuwa siyo waaminifu na hivyo fedha hazilipwi kwa wakati. Jambo hili huathiri mzunguko wa fedha kwenye biashara na kupelekea biashara kuyumba na hata kufa.
Usitengeneze utamaduni wa kukopesha kwenye biashara yako. Hata kama wengine wanafanya hivyo, wewe tengeneza wateja watakaoipenda na kuiheshimu biashara yako kiasi cha wao kuwa tayari kulipa pale wanapofanya manunuzi.

5. Kutafuta faida ya haraka.
Wafanyabiashara pia wamekuwa wakihadaika na njia za kupata faida ya haraka kwa muda mfupi. Lakini njia hizo zimekuwa haziwaachi salama, hasa baada ya muda wa faidia kuisha. Wengi wanajikuta wameingia kwenye mambo yanayoharibu sifa zao au hata kuvunja sheria. Kwa njia hii biashara inashindwa kwenda.
Unapokuwa kwenye biashara, epuka kabisa kutafuta njia ya mkato. Ijue misingi ya mafanikio kwenye biashara, na ifuate misingi hiyo. Kitu chochote nje ya msingi, achana nacho, hata kama kila mtu anafanya.
Acha mara moja kutengeneza changamoto kwenye biashara yako, biashara yenyewe ni changamoto, kuongeza nyingine ni kutengeneza njia ya uhakika ya kushindwa kwenye biashara.

 # u & me 
Read More
      edit
Published 7/01/2017 02:07:00 PM by

ABAKWA SIKU YA HARUSI YAKE



Lilikuwa janga la kwanza kati ya mawili kumkabili muhubiri huyo kijana .Lakini ni manusura.
Harusi iliopangwa ilitarajiwa kuwa harusi kubwa.
Nilikuwa muhubiri hivyobasi wanachama wote wa kanisa walitarajiwa kuhudhuria.
Mchumba wangu ,Harry na mimi tulikuwa na furaha tulikuwa tunafunga ndoa katika kanisa la All Saints Cathedral mjini Nairobi na nilikuwa nimekodisha rinda zuri sana la harusi.
Lakini usiku kabla ya ndoa yetu ,niligundua kwamba nina baadhi ya nguo za Harry .
Hakuweza kuja katika harusi bila tai kwa hivyo rafiki yangu mmoja ambaye alikuwa amekubali kubaki nami usiku wa kuamkia harusi alikubali kumpelekea mapema alfajiri.
Haki miliki ya picha Terry Gobanga Image caption Terry Gobanga
Niliamka mapema na kumpeleka hadi katika kituo cha kupanda basi.
Nilipokuwa nikirudi nyumbani ,nilipita karibu na mtu mmoja ambaye alikuwa ameketi kati boneti ya gari na akanishika kutoka nyuma na kuniingiza katika viti vya nyuma vya gari hilo na kuondoka mahali hapo.
Yote haya yalifanyika katika chini ya sekunde moja .Nilifunguliwa mdomo na kuwekwa kipande cha nguo mdomoni.
Nilikuwa nikirusha mikono na miguu nikitaka kupiga kelele.Nilipofanikiwa kutoa kitambara hicho nilipiga kelele: Ni siku yangu ya harusi! hapo ndipo nilipopigwa ngumi .
Mmoja ya wanaume hao wakaniambia nishirikiane nao ama niuwawe.Wanaume hao walinibaka kwa zamu .

Nilihisi nitafariki ,lakini bado niliendelea kupigania uhai wangu, hivyobasi mtu mmoja alipotoa kitambara kilichokuwa mdomoni mwangu nilimuuma uume wake.

CHANZO: ISHI KISTAA
Read More
      edit
Published 7/01/2017 01:44:00 PM by

KAJALA AFUNGUKIA MIMBA YAKE KUTOKA



MIEZI kadhaa iliyopita, mkali wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’ aliripotiwa kunasa ujauzito ambao uligeuka matangazo kwenye baadhi ya akaunti za Instagram, lakini hivi karibuni alionekana akiwa hana kitumbo wala kitambi, jambo lililomlazimu mwanahabari wetu kumhoji kulikoni kuyeyuka kwa mimba na kueleza ilivyotoka.
Katika majibu yake, Kajala alidai kuwa, kibendi chake kilichoropoka baada ya kupata uvimbe mkubwa tumboni.
Ishu ya Kajala kuwa mama kijacho ilienea kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ambapo aliorodheshwa kwenye listi ya mastaa wenye ujauzito Bongo.


Habari za ujauzito wa Kajala ziliambatanishwa na picha zilizomuonesha akiwa mnene, jambo alilolikwepa kwa kuwa hapendi kuongezeka mwili ndicho kigezo kilichotumika kujulikana mapema kuwa ‘ameshiba’. Baada ya ishu hiyo kusambaa, wengi walikuwa wakiandika stori za kutaka kujua mwanaume aliyempachika Kajala kibendi huku mwenyewe akiweka ngumu kumuanika.

Hata hivyo, kadiri siku zilivyosonga, joto la mimba ya Kajala lilikuwa likishuka kidogokidogo hadi kufi kia nyuzi sifuri baada ya kuonekana akijiachia kwenye viota vya burudani akiwa amevaa nguo za kumbana, kuashiria kuwa hakuwa tena na ujauzito kama watu walivyokuwa wakisema.
Katika mahojiano na gazeti hili nyumbani kwake, TRAMwenge jijini Dar, juu ya sintofahamu ya jambo hilo, Kajala alikiri kupata ujauzito, lakini haukuwa riziki kwani alikuwa na uvimbe mkubwa tumboni uliosababisha ujauzito huo kuchoropoka. “Unajua huwezi kumuelezea kila mtu nini kimekupata kwa sababu mambo mengine ni ya kibinafsi zaidi, lakini ukweli ni kwamba uvimbe ulisababisha mimba yangu kutoka na hiyo nilijua baada ya kwenda Hospitali ya Aga Khan (Dar) kufanya vipimo,” alisema Kajala.
Staa huyo aliongeza kuwa, pamoja na uvimbe kuwa sababu kubwa, pia mazoezi nayo yalichangia ambapo baada ya kukumbwa na tatizo hilo daktari alimshauri kupumzika mazoezi kwa muda.

“Pamoja na kwamba uvimbe ulikuwa ndiyo sababu kubwa, lakini daktari alinishauri hata mazoezi nipumzike kwa muda kwanza ndiyo nitaendelea nafi kiri na kunenepa ndiyo kukaongezeka,” alisema Kajala ambaye bado aliendelea kufanya siri juu ya mwanaume aliyesababisha ujauzito huo. Kajala ni mama wa mtoto mmoja wa kike aitwaye Paula Paul aliyezaa na Bosi wa Bongo Records, Paul Mathyasse ‘P-Funk Majani’

CHANZO: GPL
Read More
      edit